News

Music

Makala

Sokkaa

Video

» » Mkuu wa polisi auawa nchini Misri


Mashambulizi dhidi ya polisi Misri yamekuwa yakiongezeka
Brigedia Jenerali wa jeshi la polisi nchini Misri ameuawa katika milipuko miwili tofauti iliyotokea kwa wakati mmoja karibu na chuo kikuu cha Cairo.
Vyombo vya habari vinasema kuwa watu wengine wanne walijeruhiwa katika mashambulizi hayo.
Kwa mujibu wa maafisa wa usalama, mabomu yalikuwa yametegwa karibu na kituo cha polisi.
Hauna kundi lolote limekiri kufanya mashambulizi hayo.
Misri imekuwa ikikumbwa na mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya taasisi za serikali yanayofanywa na makundi ya wapiganaji hasa baada ya kupinduliwa kwa aliyekuwa Rais Mohammed Morsi mwezi Julai.


Chanzo BBC


Mwananchi Kweli

Tunakushukuru kwa kuendelea kusoma habari zetu tunakuomba kama unapatwa na tatizo lolote hapa kwenye tovuti yetu una maoni,Habari na ushauri usisite kutuandikia kwenye info@news4timeblog.com kisha tutakujibu haraka iwezekanavyo.Hasante.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

Leave a Reply

Select Menu