News

Music

Makala

Sokkaa

Video

» » » Rose Muhando aomba radhi!



Brighton Masalu
MWIMBAJI nyota wa nyimbo za Injili, Rose Muhando, amewaomba radhi watu wote aliowahi kuwakwaza, ikiwa ni pamoja na kuchukua fedha za kushiriki onesho, lakini akashindwa kufanya hivyo, akidai ni ubinadamu.
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, Rose alikiri kuingia baadhi ya mikataba na kushindwa kuitekeleza, akisema ni jambo lililomkosesha sana raha, hasa pale watu walipokuwa wakimchukulia kama tapeli.

“Hata hivyo, mara nyingi huwa nasingiziwa, lakini nakaa kimya kwa sababu nimeumbwa hivyo, kama kuna yeyote nimemdhulumu naomba anisamehe, sikufanya makusudi, nilishindwa kutokea kwa bahati mbaya, mimi ni binadamu. Namuomba pia baba yangu mlezi Msama (Alex, Meneja wake) naye kama kuna mahali nilimkwaza kwa matamshi au matendo, naomba anisamehe,” alisema nyota huyo wa kibao cha Facebook.

Chanzo GPL

Mwananchi Kweli

Tunakushukuru kwa kuendelea kusoma habari zetu tunakuomba kama unapatwa na tatizo lolote hapa kwenye tovuti yetu una maoni,Habari na ushauri usisite kutuandikia kwenye info@news4timeblog.com kisha tutakujibu haraka iwezekanavyo.Hasante.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

Leave a Reply

Select Menu