News

Music

Makala

Sokkaa

Video

» » » » Hili ndilo Kundi la kifo kwa watia Nia kupitia CCM


Baada ya makada kumaliza kurejesha fomu za kuomba kugombea urais kwa tiketi ya CCM jana, macho sasa yanaelekezwa kwenye vikao vya juu vya chama hicho vitakavyotoa majina yasiyozidi matano yatakayokwenda kupigiwa kura na Mkutano Mkuu utakaofanyika Julai 11 na 12.

CCM imeshatangaza kuwa itatumia vigezo 13 ilivyojiwekea kuwachambua wagombea 41 waliochukua na kurejesha fomu ili kupata majina ya wachache watakaopigiwa kura na mkutano huo mkuu, lakini Kamati ya Wazee, ambayo itatoa ushauri utakaokuwa msingi wa uamuzi wa vikao vingine na Kamati Kuu, italazimika kuangalia sifa za ziada katika kuchuja watangazania hao.

Kamati ya Wazee, inayohusisha wenyeviti na makamu wao wa zamani wa CCM pamoja na marais wa zamani wa Zanzibar, imeripotiwa kuanza kazi ya uchambuzi na itawasilisha taarifa yake kwa Kamati Kuu itakayokutana Julai 9 na baadaye kupeleka mapendekezo yake kwenye Halmashauri Kuu, ambayo huandaa ajenda za Mkutano Mkuu.

Wakati vikao hivyo vikiandaliwa, uzoefu unaonyesha kuwa CCM huzingatia mambo mengi katika kufanya uchambuzi, ikiwa ni pamoja na uteuzi wa mtu atakayeondoa makundi yaliyoundwa wakati wa kuelekea uteuzi wa mgombea urais wake, kuzingatia Muungano, jinsia, eneo la kijiografia, rekodi ya mtiania, mustakabali wa uongozi wa chama na kukubalika kwa kada, hasa katika kipindi hiki ambacho upinzani umeongezeka nguvu.

“Kuna katiba za aina mbili,” alisema mmoja wa makada ambaye aliomba jina lake lisitiriwe. “Katiba ya maandishi ambayo inatoa mwongozo wa kisheria wa namna ya kumpata Rais wa nchi, lakini pia kuna katiba ya kimtazamo ambayo si rasmi, bali ni fikra za watu wanapozungumzia aina ya rais wanayemfikiria.

“Mfano, kama kuna eneo fulani halijawahi kutoa kiongozi wa nchi, kipindi hiki sasa ni chao.”

Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Mwananchi uliojumuisha mahojiano na baadhi ya makada wenye uzoefu na mchakato wa uchaguzi ndani ya CCM, mgombea wa chama hicho tawala anaweza kutoka katika makundi manne ambayo gazeti hilo limeyaita kundi la kifo, kundi la mteule mbadala, kundi la vijana na wanawake.

Iwapo mteule hataweza kutoka kwenye kundi la kifo, ambalo linajumuisha makada wenye nafasi kubwa ya kupitishwa, chama hicho kinaweza kuamua kuchukua mwanachama ambaye atatoka kundi la wateule mbadala kwa lengo la kuzika makundi makubwa yaliyozuka wakati huu, au kuteua kada kijana iwapo CCM itakuwa inataka mwelekeo mpya, au mgombea mwanamke kama ilivyokuwa mwaka 2010 ilipoamua kuachana ghafla na Samuel Sitta na kumweka mbele Anne Makinda kuwa Spika wa Bunge, kwa maelezo kuwa umefika wakati wa wanawake.


Kundi la kifo

Kwa mujibu wa wachambuzi hao, kundi la kifo linaweza kuwa na makada sita ambao ni Profesa Mark Mwandosya, Steven Wasira, Frederick Sumaye, Edward Lowassa, Bernard Membe na Mizengo Pinda.

Katika kundi hilo, Mwandosya amekuwa hahusishwi na kashfa wala kuwa na migogoro na makada wengine. Aligombea kwa mara ya kwanza mwaka 2005 na kushika nafasi ya tatu, akiwa nyuma ya Jakaya Kikwete, aliyeshinda na Dk Salim Ahmed Salim.

Pamoja na kutokuwa na mivutano na watu, Profesa amekuwa hasikiki kutokana na kupewa kazi inayomweka mbali na wananchi.

Zaidi soma  <<<< HAPA>>>>

Mwananchi Kweli

Tunakushukuru kwa kuendelea kusoma habari zetu tunakuomba kama unapatwa na tatizo lolote hapa kwenye tovuti yetu una maoni,Habari na ushauri usisite kutuandikia kwenye info@news4timeblog.com kisha tutakujibu haraka iwezekanavyo.Hasante.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

Leave a Reply

Select Menu