Dodoma. Hali tete ndani ya ukumbi wa Bunge jana iliendelea kutanda wakati Spika Anne Makinda alipolazimika kuahirisha kikao asubuhi kutokana na kelele na baadaye chombo hicho kuwaadhibu wabunge saba wa upinzani, wakiwamo watano waliozuiwa kuhudhuria hadi kumalizika kwa Bunge la 10.
Hali hiyo ndani ya Bunge iliendelea kwa siku ya pili mfululizo na mara zote kusababisha Spika kuahirisha vikao baada ya shughuli za Bunge kushindwa kuendelea kutokana na kelele za wapinzani wanaopinga kitendo cha uongozi kuwasilisha miswada mitatu kwa hati ya dharura wakidai hakuna haja ya haraka hiyo.
Jana Spika Makinda, ambaye aliwahi kukumbana na hali kama hiyo wakati wa mjadala wa sakata la Akaunti ya Escrow kwenye Bunge la 18, aliibuka na dawa mpya na kuitumia Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuwaadhibu wabunge hao saba.
John Mnyika, Moses Machali, Tundu Lissu, Felix Mkosamali na Paulin Gekul, ambao wamekuwa wakipinga hoja mbalimbali za Serikali ikiwa ni pamoja na miswada mitatu iliyotakiwa kuwasilishwa kwa dharura kuanzia jana, wamefungiwa kushiriki vikao kuanzia leo hadi Bunge litakapovunjwa Julai 9.
Wabunge wengine wawili, Mchungaji Peter Msigwa na Rajab Mbarouk wamefungiwa kushiriki vikao viwili kuanzia leo baada ya Kamati hiyo kuwatia hatiani wawakilishi hao wote saba kwa kudharau mamlaka ya Spika.
Wengine watatu, Joseph Selasini, Khalifa Suleiman Khalifa na Rajabu Abdalah wanatakiwa kufika mbele ya kamati hiyo leo saa 4:00 baada ya wito wa kuwataka wahudhurie jana kuchelewa.
Mchungaji Msigwa, ambaye ni mbunge wa Iringa Mjini, alisema hata angefungiwa kushiriki vikao vyote, asingeathirika.
Maelezo zaidi Soma <<<<<HAPA>>>>>
Maelezo zaidi Soma <<<<<HAPA>>>>>
No comments