News

Music

Makala

Sokkaa

Video

» » Operesheni ya kijeshi yaanza katika mji wa Slovyansk

Jeshi la Ukraine linaripotiwa kuanza operesheni ya kijeshi kuudhibiti mji wa Mashariki mwa Ukraine wa Slovyansk.Kuna taarifa kuwa helikopta moja imedunguliwa katika mji huo

Shirika la habari la Ujerumani Dpa limeripoti kuwa helikopta mbili za kijeshi zimedunguliwa na rubani mmoja ameuawa huku mwingine akitekwa nyara.Waasi wanaotaka kujitenga kwa eneo la mashariki mwa Ukraine na kujiunga na Urusi wamesema wanajeshi hao wameanzisha kile walichokiita operesheni kubwa katika mji wa Slovyansk.Milio ya risasi na miripuko imesikika viungani mwa mji huo.Serikali ya Ukraine haijazungumzia operesheni hiyo ya kijeshi iliyoanza muda mfupi uliopita.Mengi zaidi kuhusu hali inavyojiri mashariki mwa Ukraine ni hivi punde.
Mwandishi:Caro Robi/dpa/Dw



Mwananchi Kweli

Tunakushukuru kwa kuendelea kusoma habari zetu tunakuomba kama unapatwa na tatizo lolote hapa kwenye tovuti yetu una maoni,Habari na ushauri usisite kutuandikia kwenye info@news4timeblog.com kisha tutakujibu haraka iwezekanavyo.Hasante.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

Leave a Reply

Select Menu