News

Music

Makala

Sokkaa

Video

» » Mvua yailazimisha DAWASCO kuzima mitambo ya maji




Shirika la Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) limezima mitambo miwili ya uzalishaji maji kwenye mitambo yake ya Ruvu Juu uliopo Mlandizi, mkoani Pwani na Mtoni uliopo Temeke, Dar es Salaam.


Hatua ya DAWASCO imetokana na mvua kubwa zilizonyesha kusababisha madhara mbalimbali katika miji ya Kibaha, Pwani na Dar es Salaam.

Taarifa ya DAWASCO kwa vyombo vya habari jana ilisema sababu za kuzimwa kwa mitambo hiyo ni bomba la kupooza mtambo wa kuchota maji yanayotoka mtoni (cooling pipe) kuharibiwa na mafuriko namitambo ya kusukuma maji kutoka kwenye chanzo cha maji (Mto Kizinga) kuwepo ndani ya maji.

Taarifa hiyo ilieleza kutokana na sababu hizo maeneo yatakayokosa huduma ya maji ni Kijichi, Mbagala Zakheam, Mtoni kwa Azizi Ally, kwa Kabuma, Azimio Kaskazini na Kusini, Wailes, Mwembe-Yanga, Sudan, Mivinjeni na Mtoni Sabasaba. Maeneo mengine ni Mlandizi, Kibaha, Kibamba, Mbezi, Kimara, Ubungo, Chuo Kikuu, Kibangu, Riverside, Barabara ya Mandela, Tabata na Segerea.

“DAWASCO inawaomba wananchi radhi kwa usumbufu utakaojitokeza … kazi itaanza baada ya mafuriko kupungua Ruvu Darajani na Mto Kizinga,” ilieleza taarifa hiyo. ---
 Tanzania Daima



Mwananchi Kweli

Tunakushukuru kwa kuendelea kusoma habari zetu tunakuomba kama unapatwa na tatizo lolote hapa kwenye tovuti yetu una maoni,Habari na ushauri usisite kutuandikia kwenye info@news4timeblog.com kisha tutakujibu haraka iwezekanavyo.Hasante.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

Leave a Reply

Select Menu