News

Music

Makala

Sokkaa

Video

» » » Hizi ndizo Jumbe za mwisho kati ya wanafunzi na wazazi wao muda mfupi kabla ya meli kuzama

Inasikitisha: Jumbe za mwisho kati ya wanafunzi na wazazi wao muda mfupi kabla ya meli kuzama

Wizara ya ulinzi utawala wa umma ya Korea Kusini imetoa ripoti leo (Ijumaa) asubuhi kuwa watu 20 ndio waliothibitika kufariki na watu 276 wamepotea kufuatia kuzama kwa meli iliyobeba idadi kubwa ya wanafunzi.
Jana zilitolewa jumbe za simu walizutimiana wazazi na wanafunzi waliokuwa kwenye meli hiyo na kati ya jumbe zilizoripotiwa ni kati ya Shin Young-Jin aliyemtumia mama yake lakini kwa bahati nzuri aliokolewa kutoka katika meli hiyo.
Shin Young-Jin: Huenda hii ndio mara yangu ya mwisho kukuambia kuwa nakupenda
Mama: “na mimi nakupenda mwanangu,” alijibu bila kufahamu nini kilikuwa kinaendelea.
Hata hivyo wengine waliopokea jumbe kama hizo bado hawajawapata watoto wao.
Shirika la AFP, limeripoti jumbe nyingine zilizotumwa:  
Mwanafunzi: "baba usijali, nimevaa boya la kujiokoa na niko na wasichana wenzangu. Tuko ndani ya meli na bado hatujaanza kuokolewa.''
Baba: Najua msaada uko njiani , lakini kwa nini hamjaanza kuelea, tafadhali jaribu kuondoka ndani ya meli kama unaweza.''
Mwanafunzi: ''Kuna msongamano mkubwa na meli tayari imeanza kuzama''
Mawasiliano mengine ni kati ya mwanafunzi mmoja na kaka yake:
Mwanafunzi: "meli imekwama na haisongi walinzi wa baharini wameanza kuwasili kujua hitilafu imetokana na nini'
Kakake:'' usiwe na wasiwasi. Fanya kila mnachoamrishwa kufanya na kila kitu kitakuwa shwari.''
Hakukuwa na mawasiliano mengine baada ya hapo na mwanafunzi huyo hajapatikana.




Mwananchi Kweli

Tunakushukuru kwa kuendelea kusoma habari zetu tunakuomba kama unapatwa na tatizo lolote hapa kwenye tovuti yetu una maoni,Habari na ushauri usisite kutuandikia kwenye info@news4timeblog.com kisha tutakujibu haraka iwezekanavyo.Hasante.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments

Leave a Reply

Select Menu