Tukio la kusikitisha la vifo vya watoto watatu wenye umri wa miaka 6, 9 na 10 lililotokea hapo jana Jumapili, Aprili 27, 2014 majira ya saa 11 jioni katika bwawa la kuogelea la hoteli ya Landmark ya Mbezi Beachi jijini Dar es Slaam limesababisha kukamatwa kwa mfanyabiashara Mboka David (44) mkazi wa Kijitonyama -- aFikra Pevu imeripoti.
Habari zilizopatikana jana kutoka kwa kwa marafiki kupitia mawasiliano ya simu zilifahamisha kuwa watoto hao waliokumbwa na masaibu hayo walichukuliwa bila ya kutoa taarifa kwa wazazi wao na kupelekwa katika hoteli hiyo kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya kutimiza mwaka mmoja wa kuzaliwa ya mtoto mwingine.
Watoto hao walipoteza uhai walipozama katika bwawa hilo kwa kushindwa kuokolewa pale walipopiga kelele kuomba msaada.
No comments